Psalms 44:1-6

Kuomba Ulinzi Wa Mungu

(Kwa Mwimbishaji: Utenzi Wa Wana Wa Kora)


1 aEe Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,
baba zetu wametueleza
yale uliyotenda katika siku zao,
siku za kale.

2 bKwa mkono wako uliwafukuza mataifa
na ukawapanda baba zetu,
uliangamiza mataifa
na kuwastawisha baba zetu.

3 cSio kwa upanga wao waliipata nchi,
wala si mkono wao uliwapatia ushindi;
ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume,
na nuru ya uso wako,
kwa kuwa uliwapenda.


4 dWewe ni mfalme wangu na Mungu wangu,
unayeamuru ushindi kwa Yakobo.

5 eKwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu;
kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu.

6 fSiutumaini upinde wangu,
upanga wangu hauniletei ushindi;
Copyright information for SwhKC